Sherehe za ufunguzi zilihudhuriwa na maafisa kadhaa, akiwemo Ibrahim Bu Milha, mshauri wa Mtawala wa Dubai kwa Masuala ya Utamaduni na Kibinadamu na mwenyekiti wa Tuzo ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Dubai (DIHQA).
Wahifadhi Qur'ani kutoka nchi 60 wanashiriki katika toleo la mwaka huu, ambalo litaendelea hadi Ijumaa, Septemba 22.
Mashindano hayo hufanyika katika vipindi viwili vya asubuhi na alasiri kila siku.
Siku ya Jumamosi, wawakilishi wa Misri, Bahrain, Malaysia, Austria na Singapore walijibu maswali ya jopo la majaji.
Jopo hilo linajumuisha wataalamu wa Qur'ani kutoka nchi mwenyeji pamoja na Misri, Oman, Bahrain, Saudi Arabia na Syria. Wajumbe wake watatu ni wataalamu wa Qur'ani wanawake.
DIHQA kila mwaka huandaa hafla ya kimataifa ya Qur'ani kwa wanawake kutoka nchi mbalimbali.
4169236