Dua hizi za kila siku za Mwezi wa Ramadhani husomwa toka mwanzo ya tarehe mosi Ramadhani hadi siku ya mwisho katika mwezi huu mtukufu. Kila dua ina siku yake, na inaweza kusomwa mara nyingi kadiri ya uwezo wa mtu mwenyewe.
Ee Mwenyezi Mungu! Ninakuomba katika mwezi huu (Unijaalie niyatende) yanayokuridhisha. Na ninajilinda kwako na yanayokuudhi. Na ninakuomba kuniwafikia katika mwezi huu nikutii pasina kukuasi, Ee mpaji wa wakuombao.