IQNA

Wanafunzi Waafrika mjini Najaf, watembezwa maeneo matakatifu kote Iraq

15:21 - February 22, 2022
Habari ID: 3474959
TEHRAN (IQNA)-Idara ya Mfawidhi wa Haram ya Hadhrat Abbas AS katika mji wa Karbala, Iraq imeandaa mpango maalumu kwa ajili ya wanafunzi Waafrika wanaosoma katika vyuo vya Kiislamu mjini Najaf.

Tovuti ya al-Kafeel imeripopti kuwa, mpango huo ambao ulianza Alhamisi iliyopita unajumuisha kutembelea maeneo mbali mbali matakatifu nchini Iraq.

Sheikh Saad al-Shimri, mkurugenzi wa Kituo cha Masomo ya Afrika katika Idara ya Mfawidhi wa Haram ya Hadhrat Abbas (AS) amesema tayari wanafunzi hao wameshatemeblea haram takatifu za Imam Hadi AS na Imam Askari AS eneo la Samarra na Imam Musa Kadhim AS na Imam Jawad AS huko Kadhimiya.

Mbali na kutekeleza ziara wanafunzi hao pia wamekutana na kufanya mazungumzo na wasimamizi wa maeneo hayo matakatifu.

Al Shimri amesema wanafunzi hao wamekaribisha mpango huo ambao umewapa fursa ya kutembelea maeneo ya kidini katika miji mbali mbali ya Iraq.

 

Kishikizo: iraq wanafunzi waafrika
captcha